Nikiamini wewe ni mzima wa afya,
karibu sana katika ukurasa huu ambao unakupa habari za kuvutia kuhusu
michezo mbalimbali inayoendelea kila siku ulimwenguni. Binafsi mimi ni
mzima na leo nimejaaliwa kukuletea
wachezaji ambao walilelewa na Manchester United tangu wakiwa wadogo lakini baadae wamekwenda kupata mafanikio sehemu nyingine kabisa. Bila kukuchosha tazama wachezaji hawa hapa chini, karibu sana…..
wachezaji ambao walilelewa na Manchester United tangu wakiwa wadogo lakini baadae wamekwenda kupata mafanikio sehemu nyingine kabisa. Bila kukuchosha tazama wachezaji hawa hapa chini, karibu sana…..
RYAN SHAWCROSS
Mchezaji huyu alizaliwa miaka 27
iliyopita kule Jijini Chester mpakani mwa nchi ya Wales na hatimaye
mwaka 2002 alitimkia Old Trafford ambapo alianza maisha yake ya soka
jijini Manchester na kukaa klabuni kwa muda wa miaka sita kabla ya
kwenda kutafuta maisha ya soka kule Royal Antwerp. Baada ya kukaa msimu
mmoja kwenye klabu hii, hatimaye Stoke City walivutiwa na huduma ya
mchezaji huyu na kumvuta Britania Stadium ambapo jezi namba 17 ilikuwa
halali yake. Shawcross amekuwa muhimili mkubwa sana katika timu yake ya
Stoke City kwa muda mrefu sasa.
Miongoni mwa mafanikio aliyopata
nje ya Old Trafford ni pamoja na kuchukua tuzo ya mchezaji bora wa klabu
ya Stoke City kwa mwaka wa 2014. Inawezekana Ryan angeweza kucheza
vyema kwenye idara ya ulinzi ya United kama angeaminiwa na kupewa nafasi
hasa baada ya kupata uzoefu kwenye EPL kabla ya kusajiliwa na Stoke
City mwaka 2008. Hadi kufikia hatua ya kuaminiwa na kupewa kitambaa pale
Britania sio kitu chepesi kama watu wanavyodhani.
DANNY WELBECK
Ni vigumu sana kuamini kama ipo
siku mchezaji huyu aliyekaa miaka 13 Old Trafford angeweza kuondoka
United na kwenda London kwa mahasimu wakubwa wa Man U, Arsenal. Welbeck
ni mchezaji anayeweza kukupa vitu viwili kwa wakati mmoja kwani hakuna
asiyefahamu kuwa huyu ni kiungo mshambuliaji mzuri mbali na kuweza
kucheza nafasi ya ushambuliaji ambayo mara kadhaa Sir Alex Fergurson
alimchezesha.
Baada ya kuondoka United, Danny
alifanikiwa kuwaonesha United kuwa hawakupaswa kumuachia kienyeji hasa
pale alipofunga ‘hat-trick’ kwenye mechi ya ligi ya mabingwa dhidi ya
Galatasaray. Pia Welbeck alifunga goli la ushindi na kuitoa nje ya
mashindano ya FA timu yake ya zamani ya United. Inawezekana tatizo la
safu ya ushambuliaji linaloikabili United kwa sasa lingepata suluhisho
japo sio la moja kwa moja endapo Welbeck angebaki jijini Manchester.
RON-ROBERT-ZIELER
Huyu ni mlinda mlango kutoka
taifa la Ujerumani na alikuwa miongoni mwa wachezaji walioiwakilisaha
Ujerumani kwenye michuano ya kombe la dunia japokuwa hakucheza mechi
yoyote. Ron alisajiliwa na United tangu mwaka 2005 kabla ya 2010 kwenda
Hannover 96 ambapo alipata nafasi ya kuonesha kiwango chake. Kwa kipindi
alichokuwa United, ilimuwia vigumu kuonesha kiwango chake hasa kutokana
na ukweli kuwa akina Edwin Van Desar walikuwa na uhakika wa kucheza
muda wote.
Inawezekana United wangethamini
kiwango cha kinda huyu wasingehangaika sana kutafuta walinda milango wa
kuziba nafasi ya De Gea endapo ataondoka. Ron ameiwakilisha Ujerumani
katika ngazi zote za vijana kabla ya mwaka 2011 kuitwa rasmi kwenye timu
ya taifa ya wakubwa.japokuwa hakuonekana kwenye kikosi cha kwanza
kilichochukua ya kombe la dunia mwaka jana ila bado anajivunia kuwa
miongoni mwa wachezaji waliovaa medali hiyo.
GIUSEPPE ROSSI
Kabla ya kwenda kwa mkopo
Newcastle mwaka 2006, mchezaji huyu alikuwa pale Old Trafford tangu
mwaka 2004 akiwa na miaka 17. United hawakuthamini kipaji chake na
kufikia hatua ya kumtoa kwa mikopo
kwenye vilabu kadhaa vikiwemo vile vya Newcastle na Parma kabla ya
Villareal kunasa saini yake mwaka 2007 ambapo alikaa hapa kwa miaka takribani sita. Akiwa Hispania alifanya makubwa na hata Babu Fergurson kufikia hatua ya kutamani kumrudisha Old Trafford. Msimu wake wa kwanza mshambuliaji huyu alifunga magoli nane kwenye UEFA na kuanza kutiliwa mashaka na mabeki kibao.
Miongoni mwa mafanikio aliyoyapata nje ya United ni yale ya
kufunga magoli 32 kwenye mechi 56 alicheza pale Villareal. Pia baada ya
kuhamia Fiorentina, Rossi alifunga magoli 14 ndani yamechi 18 alizocheza
licha ya majeruhi kumuandama mara kwa mara. Japokuwa anapata majeraha
ya mara kwa mara, Rossi bado ameiwakilisha timu yake ya taifa mara 30 na
kufunga magoli 7 huku muda mwingi akitokea benchi.kwenye vilabu kadhaa vikiwemo vile vya Newcastle na Parma kabla ya
Villareal kunasa saini yake mwaka 2007 ambapo alikaa hapa kwa miaka takribani sita. Akiwa Hispania alifanya makubwa na hata Babu Fergurson kufikia hatua ya kutamani kumrudisha Old Trafford. Msimu wake wa kwanza mshambuliaji huyu alifunga magoli nane kwenye UEFA na kuanza kutiliwa mashaka na mabeki kibao.
GERALD PIQUE
Miongoni mwa wachezaji waliopata
mafanikio hasa baada ya kuondoka Old Trafford ni ‘Baba Shakira’ Huyu
jamaa licha ya kusajiliwa kwa mkopo Real Zaragoza, bado alikuwa
anamilikiwa na United kabla ya kusajiiwa na Barcelona mwaka 2008. Pique
hakuonekana sana pale United kutokana na uwepo wa John Oshea na makosa
yake madogo madogo ambayo hadi leo yanaonekana pale Camp Nou.
Wachambuzi wengi wa soka walitegemea Pique lazima angeondoka Old
Trafford hasa baada ya Fergurson kutovutiwa sana na uchezaji wake.
Tunapozungumzia mafanikio aliyoyapata Gerald Pique baada ya
kumpa mkono wa kwaheri Sir Alex Fergurson, ni yale ya kuchukua vikombe
kibao akiwa na Barcelona, vikombe ambavyo asingevipata kama angebaki
nchini Uingereza. Pique pia amefanikiwa kuiwakilisha vyema timu yake ya
taifa hadi kuchukua kombe la dunia na lile la Euro. Mafanikio haya
ameyapata baada ya kucheza kwa mafanikio pale FC Barcelona na hatimaye
kuaminiwa na kocha wa timu ya taifa ya Hispania.
PAUL POGBA
Nina uhakika Manchester United
wanajuta hadi leo pale wanapomuona Pogba akifanya yake katikati ya
uwanja. Kiungo huyu muhimu alikaa kwa muda wa miaka 2 pale kwenye
Academy ya Manchester United kabla ya kupandishwa kwenye timu ya wakubwa
mwaka 2012. Hatimaye Juventus walinasa saini yake na kumpa nafasi ya
uhakika kikosini kitu ambacho kilimfanya aiwakililishe Ufaransa kwenye
ngazi zote za vijana na hata
timu ya taifa ya wakubwa. Hakuna anayebisha juu ya kiwango cha mchezaji huyu anayewindwa na timu za Chelsea na FC Barcelona. Mafanikio aliyopata baada ya kuondoka pale United ni makubwa mno kulingana na umri wake. Nadhani mnakumbuka kwenye michuano ya kombe la dunia iliyomalizika mwaka jana ambapo Pogba alichukua tuzo ya Mchezaji bora chipukizi wa michuano hiyo. Kama hiyo haitoshi, Pogba pia baada
ya kuisaidia Juventus kufika fainali ya UEFA, hatimaye alitwaa tuzo ya mchezaji bora chipukizi pia. Usishangae kuona dirisha lijalo Pogba akavunja rekodi ya usajili kwa kuchukuliwa na Chelsea au Barcelona.
timu ya taifa ya wakubwa. Hakuna anayebisha juu ya kiwango cha mchezaji huyu anayewindwa na timu za Chelsea na FC Barcelona. Mafanikio aliyopata baada ya kuondoka pale United ni makubwa mno kulingana na umri wake. Nadhani mnakumbuka kwenye michuano ya kombe la dunia iliyomalizika mwaka jana ambapo Pogba alichukua tuzo ya Mchezaji bora chipukizi wa michuano hiyo. Kama hiyo haitoshi, Pogba pia baada
ya kuisaidia Juventus kufika fainali ya UEFA, hatimaye alitwaa tuzo ya mchezaji bora chipukizi pia. Usishangae kuona dirisha lijalo Pogba akavunja rekodi ya usajili kwa kuchukuliwa na Chelsea au Barcelona.
No comments:
Post a Comment