Bw. Jaffar Mneke akiongea na waandishi wa habari kuhusu uzinduzi huo wa kampeni zake za ubunge huko Newala jijini Dar es Salaam Jana
Mgombea ubunge wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania kwa tiketi ya Chama cha Wananchi (CUF), Bw. Jaffar Mneke
(PICHANI) kwa jimbo la Newala Vijijini anayeungwa mkono na vyama
vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), atazindua kampuni zake
Jumapili Septemba 06, 2015 katika viwanja vya Kitangari Sokoni mjini
Kitangari.
Akizungumza jana (Alhamisi) jijini Dar es
Salaam, Bw. Mneke amesema uzinduzi huo utakaohudhuriwa na mamia ya
wananchi waliotayari kwa mabadiliko utafanyika katika viwanja hivyo
kuanzia saa 8 mchana mpaka saa 12 jioni.
Aliongeza kuwa viongozi kadhaa wa kitaifa
wa vyama vya Ukawa, mkoa na wilayani watahudhuria uzinduzi huo
nitakaoutumia pia kutambulisha kauli mbiu inayochagiza mabadiliko kwa
wana Newala isemayo “Safari ya Mabadiliko ya Kweli Newala.”
“Nitautumia mkutano huo kueleza ilani ya
Ukawa katika kuwaletea wananchi wa Tanzania na Newala mabadiliko lakini
pia kama mgombea makini wa jimbo hilo nitaeleza tatizo kubwa
linalokwamisha maendeleo ya jimbo na kuwataka wananchi waubngane nami
katika safari ya mabadiliko na kujikomboa kutoka katika tanuru la
umaskini, kero zisizokwisha na maendeleo duni,” alisema.
Katika uzinduzi huo pia wananchi
mbalimbali watapata fursa ya kuainisha kero za muda mrefu wanazotaka
Serikali na Mbunge wa Ukawa wazifanyiekazi.
Bw. Mneke ambaye kitaaluma
ni mwalimu na mwanadiplomasia anasema alipata elimu ya juu katika Chuo
Kikuu cha Mtakatifu Yohana (St. John’s University of Tanzania) ambako
alitahasusi katika masuala ya Elimu na kutunukiwa shahada ya kwanza ya
Uwalimu.
Kati ya mwaka 2013 na 2014
alijiunga na Chuo cha Diplomasia kilichopo Kurasini jijini Dar es Salaam
na kujipatia Stashahada ya Umahiri katika Diplomasia (Post-Graduate
Diploma in Management of Foreign Relations) ambako alihitimu kwa kiwango
cha mwanadiplomasia wa daraja la kwanza (first class)
Amewaambia
wanahabari kuwa pamoja na kazi mbalimbali za harakati za kuchagiza
maendeleo katika ngazi ya Taifa na kimataifa, kwa miaka kadhaa
amefanyakazi adhimu ya ualimu ambako alipanda ngazi hadi kuwahi kuwa
Makamu Mkuu wa Shule katika Shule za Sekondari za Ilala na Dar es Salaam
Islamic.


No comments:
Post a Comment