Hamisi
Kiiza ‘Diego’ (kulia) akijaribu kumtoka mchezaji wa Mwadui wakati timu
hizo zilipokutana kwenye mchezo wa kirafiki hivi karibuni
Baada ya jana kubanwa na kupokea
kichapo cha goli 2-0 kutoka kwa JKU, hatimaye Wekundu wa Msimbazi leo
wameibuka na ushindi wa goli 3-1 walipocheza mchezo wa kirafiki wa
kujipima nguvu dhidi ya Mafunzo ya Zanzibar ambayo ndio mabingwa
watetezi wa ligi kuu ya visiwani Zanzibar.
Mchezo huo ulisukumwa saa 10:00
jioni kwenye uwanja wa Amaan, Mafunzo ndio walikuwa wa kwanza
kuzifumania nyavu za Simba kipindi cha kwanza dakika ya 30 kupitia kwa
Jaku Juma akitumia vizuri pasi iliyopigwa na Haji Ramadhani na
kuukandamiza mpira wavuni.
Simba wakasawazisha bao hilo
dakika ya 36 mfungaji akiwa ni Peter Mwalyanzi, bao la pili la Simba
limefungwa na Said Issa kwa kichwa akiunganisha krosi iliyochongwa na
Awadh Juma dakika ya 43.
Hamisi Kiiza ‘Dioego’ aliifungia
Simba goli la tatu na la ushindi dakika ya 68 akitumia vyema pasi kutoka
kwa Mwinyi Kazimoto aliyeshirikiana na Mussa Mgosi kupika bao hilo.
Simba ipo visiwani Zanzibar kwa
kambi ya mwisho ya maandalizi kuelekea michuano ya ligi kuu inayotarajia
kuanza kurindima kuanzia Septemba 12 mwaka huu.
No comments:
Post a Comment