Mshambuliaji tegemezi wa Gor
Mahia, Michael Olunga yupo nchini Afrika Kusini akifanya majaribio
kwenye klabu ya Bidvest Wits inayoshiriki ligi kuu ya nchini hiyo (PSL).
Olunga alisafiri Jumatatu
kuelekea kwa Madiba kujaribu bahati yake kufuatia msimu mzuri alikuwanao
kwenye ligi ya Kenya (Kenyan Premier League) ambapo amekuwa akiifungia
timu yake magoli muhimu.
Akizungumza kupitia
supersport.com akiwa Geneva, mwenyekiti wa Gor Mahia Ambrose Rachier
amethibitisha kuwa kunamaendeleo mazuri juu ya dili hilo.
“Tumempa ruhusa Michael Olunga
kusafiri kwenda Afrika Kusini kwa ajili ya majaribio kwenye klabu ya
Bidvest Wits baada ya klabu hiyo kuwatumia maombi ya kumhitaji Olunga
kwenda kufanya majaribio”, amesema Rachier.
“Bado ni mchezaji wetu hadi 2016
na tutahusika moja kwa moja kwa lolote litakalotokea. Atakuwa huko kwa
wiki moja na tumewapa baraka zetu, Rachier aliiambia supersport.com”.
Olunga anakuwa mchezaji wa pili
kufanyiwa majaribio kwenye klabu ya Bidvest ndani ya kipindi cha wiki
moja akimfuata mfungaji anaeongoza kwa kupachika mabao kwenye ligi ya
Kenya akiwa ameshafunga mabao 19 lakini akashindwa kumshawishi kocha wa
Wits Gavin Hunt.
Olunga pia alitwaa kiatu cha
dhahabu kwenye michuano ya CECAFA Kagame baada ya kutupia nyavuni goli
tano lakini timu yake ikashindwa kuchukua kombe hilo ilipokubali kipigo
cha goli 2-0 kwenye fainali ya michuano hiyo.
No comments:
Post a Comment