Mayasa Mariwata na Shani Ramadhani
OHOOO! Wasanii wa Bongo
Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ na mwanadada Pamela Daffa
‘Pam D’ wamenaswa wakidendeka ndani ya gari la Nay aina ya Nissan
Murano.
Tukio hilo lililonaswa ‘live’ na
makachero wetu, lilijiri hivi karibuni usiku, maeneo ya Kinondoni Studio
jijini Dar ambapo makachero wetu walikuwa wakirandaranda mitaani kusaka
matukio ndipo wakakutana na tukio hilo la aibu.
Mapaparazi wetu baada ya kulibaini gari
aina ya Murano ni la Nay na limepaki uchochoroni huku ndani akiwa na
mrembo huyo wakifanya madudu yao, waliwasogelea kwa staili ya kunyata na
walipowakaribia, walipiga picha fasta kisha kutoweka eneo hilo.
Baada ya kujiridhisha kuwa Nay alikuwa
na Pam D kupitia picha hiyo, siku iliyofuata mapaparazi wetu walianza
kumtwangia simu Pam D anayetamba na ngoma ya Popolipopo ambaye alishtuka
kuambiwa picha hiyo imenaswa.
“Daah! Kumbe mlionipiga picha ni
nyinyi? Aisee nimewavulia kofia, lakini kwani tatizo liko wapi mimi kuwa
na Nay kwenye gari na kufanya yale tuliyoyafanya?,” aliwahoji
mapaparazi wetu Pamela na kukata simu.
Alipotafutwa Nay, alijibu kwa kifupi: “Niko taiti kidogo nipigie baadaye.”
Alipopigiwa tena baadaye, hakupokea.
Nay baada ya kumfumania mzazi mwenzake
Siwema miezi kadhaa iliyopita kisha kuachana naye, alizama kwenye
‘malovee’ na staa wa Bongo Movies, Shamsa Ford ambapo naye hivi karibuni
alidai wameachana na hatimaye amenaswa na Pam D.
No comments:
Post a Comment