Kiungo
wa Simba SC Joseph Kimwaga akiwa chini baada ya kupata maumivu wakati
timu yake ilipocheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Mwadui FC
Na Baraka Mbolembole, Dar es Salaam
Kiungo anaekipiga kwa mkopo
katika klabu ya Simba SC, Joseph Kimwaga amekiri wazi kuwa alikata tama
ya kucheza mpira baada ya mambo kuwa magumu katika klabu ya Azam FC.
Kimwaga licha ya kushindwa kupata nafasi katika kikosi cha kwanza cha
Azam FC alisumbuliwa na majeraha ya goti kiasi cha kufanyiwa upasuaji
nchini Afrika Kusini.
Mchezaji huyo anayertumia mguu wa
kushoto anakumbukwa na wapenzi wengi wa mpira nchini kutokana na
kufunga goli la ushindi katika mchezo wa ligi kuu Tanzania Bara dhidi ya
Yanga SC Novemba, 2013 wakati Azam iliposhinda 3-2.
“Baada ya kuumia na kuwa nje kwa
muda mrefu nilianza kukata tama kama kweli ningeweza kurudi katika
kiwango changu cha kawaida. Kusajiliwa na Simba nitachukulia kama njia
ya kurejesha makali yangu” anasema Kimwaga wakati nilipozungumza naye
kwa njia ya simu akiwa kambini Zanzibar.
“Nipo hapa kufanya kazi, lengo
langu ni kushirikiana na wenzangu kuisaidia Simba msimu huu. Najifua ili
kumshawishi mwalimu nipate nafasi ya kucheza mara kwa mara. Unajua
nimekuwa nje ya uwanja kwa mwaka mzima kutokana na majeraha. Anasema
Kimwaga ambaye tangu amepona hakuwahi kuichezea Azam FC katika gemu ya
ushindani.
No comments:
Post a Comment